Mradi wa Maji unaotekelezwa na Serikali kupitia wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) katika Kata ya Mbomole na Sakale zilizopo tarafa ya Amani Wilayani Muheza mkoani Tanga unatarajia kunufaisha zaidi ya wakazi 3700, Mradi utakaogharimu kiasi cha Tsh Milioni 800 ambapo hadi sasa ujenzi wake umefikia asilimia 72 huku ukiratajia kukamilika ifikapo 30 November 2023
Akizungumza wakati wa kuweka Jiwe la Msingi katika mradi huo, Mkuu wa Mkoa wa Tanga Waziri Kindamba amesema uwezo wa mradi huo katika Kutunza maji ni Lita laki moja na Nusu (150,000), ambapo matumizi kwa wakazi wa hapo ni lita elfu Tisini pekee ambapo hadi kufikia sasa zaidi ya Tsh Milioni 215.3 zimekwishatumika.
Category
Show more
Comments - 0
Related videos for MRADI WA MAJI WA MILIONI 877.5 KUNUFAISHA WAKAZI 3715 MUHEZA: