WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameridhishwa na hatua iliyofikiwa kwenye ujenzi wa madarasa yanayotokana na fedha za maendeleo mkoani Lindi.
Ametoa kauli hiyo leo mchana (Jumanne, Desemba 28, 2021) wakati akizungumza na viongozi wa mkoa huo kwenye uwanja wa ndege wa Nachingwea mara baada ya kupokea taarifa ya kila wilaya.